.

.

Watu wenye silaha walivamia bunge nchini Libya

Watu wenye silaha walivamia bunge nchini Libya

Watu wenye silaha jana walilishambulia bunge la Libya na kuwalazimisha wabunge kuakhirisha kupiga kura kwa ajili ya kumchagua Waziri Mkuu Mpya wa nchi hiyo.
 Wavamizi hao waliokuwa na silaha waliwajeruhi pia watu kadhaa wakati wa shambulio hilo katika bunge la taifa la Libya huko Tripoli. Hayo yameelezwa na msemaji wa Bunge Omar Hmeidan. Wavamizi hao wanasadikiwa kuwa na uhusiano na wagombea waliobwagwa katika kinyang'anyiro cha kuwania kiti cha Waziri Mkuu wa Libya
Hata hivyo shambulio hilo dhidi ya bunge la taifa la Libya lilimalizika mara moja, na kuwalazimisha wabunge kuakhirisha kupiga kura ya kumchagua Waziri Mkuu Mpya hadi wiki ijayo.
Share on Google Plus

About Dira Ya Maisha

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Chapisha Maoni