.

.

WAFAHAMU MAMA SHUJAA WA CHAKULA KUTOKA MKOA WA ARUSHA WANAOTARAJIA KUINGIA KIJIJI CHA MAISHA PLUS SIKU YA JUMAPILI WIKI HII!




ELINURU MOSES PALLANGYO (52) mkazi wa Meru Arusha, namba yake ya ushiriki ni MS 01, ni mkulima na mfugaji ana shamba la ukubwa wa robo tatu ekari, analima ndizi na mboga na kufuga ng’ombe, mbuzi na kuku.

ANADHANI YEYE NI MFANO WA KUIGWA: Anajituma na kazi yake inaonekana, watu kutoka ndani na nje ya nchi, vikundi, mashirika naa watu binafsi huwenda kujifunza katika darasa lake la kujitolea.Anasema "kwa mwaka ninavuna ndizi mikungu 70, ninapata kilo 336 za nyama za kuku pamoja na maziwa lita 3780"


DOROTHY DANIEL PALLANGYO (64) mkazi wa Meru Arusha, namba yake ya ushiriki ni MS 02 yeye ni mkulima na mfugaji ana shamba la ukubwa wa ekari 2 na anafuga ng’ombe na mbuzi.
 
ANADHANI YEYE NI MFANO WA KUIGWA:  Kwa sababu Anafuga kisasa na ana banda bora la mifugo, pia analima kwa kuotesha kwa kufuata ushauri wa kitaalamu. "nina shamba lenye ukubwa wa ekari 2. Kwa mwaka ninavuna mazao gunia 30 na ninapata lita 5,040 za maziwa"


Share on Google Plus

About Dira Ya Maisha

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Chapisha Maoni