Uchaguzi wa urais nchini Ukraine umepangwa kufanyika Mei 25, lakini waasi wa miji ya Lougansk na Donetsk mashariki mwa Ukraine wameapa kutoshiriki uchaguzi huo.
Serikali ya Kiev inaungwa mkono na mataifa ya magharibi, huko waasi waliyotangaza kujitenga na Ukraine wakiungwa mkono na Urusi.
Mapigano kati ya jeshi na waasi yanaendelea kurindima mashariki mwa Ukraine karibu mwezi moja sasa, baada ya jeshi kuanzisha operesheni dhidi ya “ugaidi”, lengo hasa ikiwa ni kurejesha mikononi mwa serikali maeneo yanayoshikiliwa na waasi mashariki mwa taifa hilo.
Hayo yakijiri katibu mkuu wa jumuiya ya kujihami ya mataifa ya magharibi Nato, Anders Fogh Rasmussen anakutana kwa mazungumzo katika mji wa Bratislava na viongozi wa Ukraine, Slovakia , Hungary, Jamhuri ya Czech na Poland. Wakati huo huo , mkuu wa ujumbe wa uangalizi wa jumuiya ya Usalama na Ushirikiano barani Ulaya (OSCE) nchini Ukraine, Ertuğrul Apakan, anatarajiwa kuhutubia leo mbele ya baraza ya jumuiya hio.
Siku moja kabla, serikali ya kiev imekabiliwa na kibarua kigumu kwa kuandaa mazungumzo ya kitaifa yaliyo washirikisha wadau wote katika usalama wa Ukraine. Marais wawili wa zamani wa Ukraine, wagombea urais, wabunge na ujumbe wa baadhi ya waasi wameshiriki mazungumzo hayo.
Lakini waasi wa miji ya Donetsk na Lougansk ambao waliopiga kura ya maoni jumapili iliyopita, hawakushiriki mazungumzo licha ya wito uliyotolewa na Urusi.
Serikali ya Kiev inaungwa mkono na mataifa ya magharibi, huko waasi waliyotangaza kujitenga na Ukraine wakiungwa mkono na Urusi.
Mapigano kati ya jeshi na waasi yanaendelea kurindima mashariki mwa Ukraine karibu mwezi moja sasa, baada ya jeshi kuanzisha operesheni dhidi ya “ugaidi”, lengo hasa ikiwa ni kurejesha mikononi mwa serikali maeneo yanayoshikiliwa na waasi mashariki mwa taifa hilo.
Hayo yakijiri katibu mkuu wa jumuiya ya kujihami ya mataifa ya magharibi Nato, Anders Fogh Rasmussen anakutana kwa mazungumzo katika mji wa Bratislava na viongozi wa Ukraine, Slovakia , Hungary, Jamhuri ya Czech na Poland. Wakati huo huo , mkuu wa ujumbe wa uangalizi wa jumuiya ya Usalama na Ushirikiano barani Ulaya (OSCE) nchini Ukraine, Ertuğrul Apakan, anatarajiwa kuhutubia leo mbele ya baraza ya jumuiya hio.
Siku moja kabla, serikali ya kiev imekabiliwa na kibarua kigumu kwa kuandaa mazungumzo ya kitaifa yaliyo washirikisha wadau wote katika usalama wa Ukraine. Marais wawili wa zamani wa Ukraine, wagombea urais, wabunge na ujumbe wa baadhi ya waasi wameshiriki mazungumzo hayo.
0 comments:
Chapisha Maoni